Monday, July 12, 2010

WATU 23 WAFA KWA MIRIPUKO KAMPALA

Milipuko imetokea katika mji mkuu wa Uganda Kampala iliyolenga mashabiki wa soka waliotizama mechi ya fainali ya kombe la dunia katika televisheni.

Idadi kamili ya waliofariki bado haijulikani japo awali miili 23 ilipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti. Duru zinaarifu kuwa idadi hiyo inahofiwa kufikia zaidi ya watu 60.

Mkuu wa polisi nchini humo Kale Kaihura amesema kuwa uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa milipuko hiyo iliyotokea katika mikahawa ya vyakula na pombe ilinuiwa kusababisha maafa zaidi, ambapo mripuko wa kwanza ulitokea kwenye mgahawa wa Kiethiopea kusini mwa mji huo mkuu, na mripuko mwengine ulitokea kwenye mgahawa wa klabu ya mchezo wa Rugby mashariki mwa Kampala.

Shaka kuu imetiliwa kikundi cha wapiganaji wa kiislamu Al-Shabab nchini Somalia ambako Uganda imetuma majeshi yake kusaidia katika shughuli ya amani chini ya muungano wa Afrika

.

No comments:

Post a Comment