Monday, July 12, 2010

TUNZO ZA ADIDAS KWA MASHINDANO YA KOMBE LA DUNIA

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Uruguay Diego Forlan ametajwa kua ndio mchezaji bora FIFA kwenye michuano ya kombe la dunia huko Afrika Kusini na kutunukiwa mpira wa dhahabu.
Forlan ametunukiwa tunzo hio ambayo inatolewa na kampuni ya Adidas baada ya kuisaidfia timu yake ya Uruguay kwa kuipatia jumla ya magoli matano na kufanikiwa kuingia katika nne bora.

Diego Forlan pia alitajwa katika jumla ya wachezaji wanaowania tunzo ya kiatu cha dhahabu, tunzo ambayo imekwenda kwa mchezaji wa taifa la ujerumani Thomas Muller.

Mchezaji wa pili aliyemfuatia Forlan ni Mchezaji kutoka timu ya taifa ya Netherlands "Oranje" Wensley Snijder ambae aliibuka na mpira wa fedha wakati mshambuliaji David Villa aliibuka na mpira wa shaba kwa kushinda nafasi ya tatu.

No comments:

Post a Comment