Sunday, July 11, 2010

MAMBO YA WAZUNGU



Picha hizi nilizipiga kipindi cha baridi na ilikua ni mwezi wa Januari mwaka huu, kwa wakati ule hapa palikua na uwanja wa mpira pamoja na mabenchi ambayo watu walikua wakikaa kipindi cha jua,lakini jamaa wameibadilisha hii sehemu na huwezi ukajua kama mwanzo hapa palikua hivi, picha za chini zinaonesha jinsi hali ya sasa uwanjani hapa ilivyo.

Hivi ndivyo hali ilivyo kwa sasa, hakuna tena uwanja wa mpira wala mabenchi ya kukalia, lakini jamaa wameweka mto wa maji ambao haukuwepo kabla, na wanatengeneza sehemu ya kuchezea watoto ambayo bado haijamaliza, uwanja huu ingelukua ni nyumbani basi wakubwa weshauchukua na kujijengea majumba yao binafsi, lakini kwa wenzetu wanajua ni jinsi gani ya kuwaridhisha wananchi wao na kujenga nchi yao, sijui hawa viongozi wetu wakija huku ulaya kila siku wanajifunza nini.

No comments:

Post a Comment