Sunday, July 18, 2010

WACHEZAJI WA UHOLANZI WAUAGA UKAPERA


Mchezaji wa Uholanzi anaecheza kwatika safu ya ulinzi John Heitinga amefunga ndoa na mwanamke anaejuilikana kwa jina la Sophie Cherlotte ambae alikua akiishi nae na kuzaa nae mtoto moja wa kike.

Heitinga na Shophie wamefunga ndoa siku ya Alhamis katika fukwe za Cap d'falco huko mjini Ibiza Uhispania.

Alipozungumza na mwandishi wa habari wa gazeti la De Telegraaf la Uholanzi Sophie alisema kwamba "John ndie ndoto yangu na kila mmoja wetu anajisikia vizuri sana". alisema Sophie huku akitokwa na machozi.

Bada ya ndoa hio kufungwa kulifanyika sherehe kubwa ambayo ndugu na jamaa wa pande zote mbili walihudhuria wakiwemo marafiki, ambapo sherehe hio ilijumuisha watu 130.

Miongoni mwa watu maarufu waliohudhuria sherehe hio ni pamoja na Rafael van der Vaart na mkewe Sylvie, Estelle Gullit, Frank de Boer na familia yake, Patty Brard na Gordon.

Lakini wachezaji wengi wa Uholanzi hawakuhudhuria harusi hio kutokana na wachezaji hao kuwepo mpumziko baada ya kumaliza kwa Kombe la Dunia.

Wakati huo huo mchezaji wa Uholanzi ambae alipata zawazi ya pili kwa uchezaji bora katika fainali za Kombe la Dunia Wensley Snijder nae amefunga ndoa na mchumba wake Yolanthe.

Snijder na Yolanthe wamefunga ndoa leo hii katika kanisa moja huko nchini Italy ambapo ndoa hio ilifanyika katika mila za Kitaliano na Kiengereza.

Ndoa hio pia ilionekana kama ni ya kifalme kwani wanandoa hao waliingia kanisani wakiwa katika gari la farasi ambalo liliendeshwa na farasi 6 na baadae ndani ya kanisa hio mtoto wa Snijder anaejuilikana kwa jina la jessey aliingia na kumletea babaake pete ya ndoa.


No comments:

Post a Comment