Monday, July 19, 2010

UKIMWI NA CHANJO

Kirusi cha ukimwi

Shamrashamra nyingi tulizisikia hivi karibuni pale watafiti wa NIH nchini Marekani walipotoa ripoti ambayo ni habari njema katika vita dhidi ya Ukimwi. Watafiti hawa wameeleza kuwa wamegundua chembechembe, yaani antibodies, zenye uwezo mkubwa wa kuzuia kirusi cha ukimwi (HIV) kuingia kwenye seli nyeupe za damu — kwa 90% — na hivyo kusitisha mazaliano ya HIV.

Pamoja na shamrashamra hizi, wengi wetu tukaanza kusikia habari potofu zikisambazwa na wanahabari Tanzania kuwa ‘Dawa ya Ukimwi yapatikana,’ na kusikia vijana wakianza kuongelea (labda kushangilia) ngono isiyo salama, πβ%ϕЖ&!!

Ukweli ni kwamba ‘dawa ya Ukimwi´ haijagunduliwa - bali huu ni mwanzo tu wa safari ndeeefu ya kufikia nia hiyo. Mwaka jana kulikuwa na mlipuko wa habari kama huu kuhusiana na chanjo ya HIV – ila angalau ile ilikuwa tayari katika utafiti wa clinical trial!


‘Twisheni’

* Sote tunafahamu kuwa miili yetu hutengeneza chembechembe dhidi ya virusi, bakteria, n.k mbalimbali na hivyo kusitisha ugonjwa wanaosababisha kuanza.

* Kirusi cha ukimwi kinauwezo wa kubadilika kwa kasi kubwa na kuzaliana kabla mwili haujatengeneza chembechembe thabiti kudhibiti mazaliano zaidi ya virusi – by the time chembechembe thabiti zikiwa tayari, kirusi nacho kinakuwa tayari kimezalisha copy nyingine nyingi tofauti (a rat race!).

* Ripoti hii mpya inaeleza ugunduzi wa chembechembe (VRCO1 na VRCO2) zenye uwezo maradufu wa kuzuia kuzaliana kwa HIV katika maabara. Chembechembe hizi zinagundua na kubana sehemu ya kirusi isiyobadilika (isiyo mutate), kwahivyo kuzuia HIV kupenya na kuzaliana ndani ya seli nyeupe za damu.

* Umuhimu wa ugunduzi huu umetokana na teknolojia mpya za molecular/computational/structural biology ambazo zilitumika ili ‘kuvua’ chembechembe hizi kutoka kwa wagonjwa wa ukimwi. Baada ya test kadhaa maabarani, ndipo chembechembe hizi zikaonyesha uwezo wake huo mkubwa wa kuzuia HIV.

Changamoto zilizopo sasa ni kufahamu: Je, chembechembe hizi zina uwezo wa kiasi gani kuzuia HIV katika mwili wa mnyama au binadamu? Pindi chanjo madhubuti itakapopatikana, chembechembe hizi zinaweza kuzalishwa kawaida mwilini na mtu yeyote asiyeathirika ili kumkinga na HIV? Ni kiasi gani cha chembechembe hizi zitahitajika kuzuia HIV kuzaliana mwilini kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa (passive immunization)? Haya ni baadhi ya maswali jumuiya ya sayansi itakabiliana nayo baada ya ripoti hii. Safari bado ni ndefu, na ni miaka kadhaa mpaka tutakapoona chanjo madhubuti dhidi ya HIV. Ila, imani bado ipo.

No comments:

Post a Comment