Tuesday, July 13, 2010

FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA BARANI AFRIKA LAZIUNGANISHA BARA ZIMA

Fainali za kwanza za kombe la dunia katika ardhi ya bara la Afrika zilipaswa kuionyesha dunia sura mpya ya bara hilo.

Ulikuwa mwezi mzima uliojaa shauku, maamuzi mabaya, shangwe nyingi, lakini ulikuwa pia mwezi uliojaa matumaini makubwa. Fainali za kwanza za kombe la dunia katika bara la Afrika, ilikuwa ishara ya matarajio makubwa katika bara hilo. Dunia ilipaswa kuona , kuwa Afrika kusini inatayarisha vizuri mashindano haya, na Waafrika walipaswa kwa ujumla kuzihimiza timu zao kusonga mbele.

Lakini mashindano ya kombe la dunia kweli yalistahili kuliunganisha bara lote na kusafisha haiba yake? Kombe la dunia ni nafasi kubwa kuweza kusafisha sura ya bara letu tukufu.

Kwa Joseph kutoka Cameronn fainali za kombe la dunia nchini Afrika kusini sio tu mchezo katika viwanja. Kijana huyo mchuuzi anazungumzia kile Waafrika wengi wanachofikiri. Haijawahi kutokea mashindano kama hayo ya kandanda kuwa na umuhimu mkubwa. Kutoka katika historia ya kutokuwa na chochote, amesema rais wa zamani wa Afrika kusini Thabo Mbeki. Katika fainali hizi za kombe la dunia mtu anaweza kukumbuka jambo moja, furaha ya Waafrika, na dhahiri ni ishara ya mapambano dhidi ya umasikini uliolizingira bara hilo kwa karne kadha pamoja na mizozo.

Sio tu Afrika kusini inaona mafanikio hayo ya kispoti kwa shauku kubwa. Bali pia nchi nyingine za bara hilo, zimeyaona mashindano hayo kuwa na umuhimu mkubwa.

Mafanikio haya yatalitumbukiza bara la Afrika katika hali mpya. Ni ahadi kwa mustakbali wa bara hilo.

Allah Anicet anaamini katika nguvu za michezo. Na pia ni makamu wa rais wa shirikisho la soka la Ivory Coast.

Michezo ina uwezo wa kuwaongoza raia. Na wale wote wasio wanasiasa. Michezo inatupa mtazamo wa pamoja sisi Waafrika. Kila mmoja hivi sasa anazungumzia kuhusu umoja wa nchi za Afrika na umoja wa Afrika. Na katika kiwango cha taifa michezo inaweza kuimarisha umoja wa kitaifa.

Hilo limeonyeshwa na Ghana , timu ya nchi hiyo ilipopambana hadi katika robo fainali. Kabla ya mchezo bara zima liliingiwa na homa, kuwaombea Black Stars kusonga mbele katika nusu fainali. Raia wa Afrika kusini waligawa bendera za Ghana bure na gazeti la Daily Sun , liliandika, Matumaini ya Afrika na ndoto yanatuwana kwa Black Stars.

Diego Forlan , mshambuliaji wa Uruguay, anakiri kwa usahihi, Tunalazimika kukabiliana na bara zima la Afrika. Na kwa wakati fulani hali ilionekana wazi, kila mmoja alikuwa na matamanio ya umoja wa Afrika nzima. Iwapo ni Ivory Coast, Cameroon ama Ghana, shauku ilikuwa haina mipaka, kama ilivyo mara zote, tangu Afrika kushiriki kwa mara ya kwanza katika fainali za kombe la dunia.

Tangu nchi ya kwanza kuwahi kufanikiwa kushiriki katika fainali za kombe la dunia, ikiwa ni Morocco mwaka 1970, kila timu ya Afrika inayofanikiwa kuingia katika fainali hizo inakuwa mwakilishi wa bara zima la Afrika.

Abdulrazak Abdulkarim , kocha na mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Ghana anaelezea kuwa,

Hatimaye watu katika bara zima la Afrika wanafurahia kandanda la Afrika. Hii ni hali nzuri kwetu sisi na hali nzuri kwa wachezaji wetu wachanga.

Nae Charles Adou, mwenye duka la dawa mjini Abidjan nchini Ivory Coast, anasisitiza jukumu walilolitekeleza timu ya Ghana katika fainali hizi za kombe la dunia, kwa kusema katika mazingira magumu Waafrika wamekuwa wapiganaji. Kama tulivyoona, vile Ghana ilivyofikia, kila mmoja alipaswa kuiunga mkono Ghana , kwamba ni timu ya kwanza , kutoka bara la Afrika kuingia nusu fainali.

Lakini ghafla, Ghana ilishindwa katika mikwaju ya penalti dhidi ya Uruguay. Na ndio timu ya mwisho ya Afrika kuondolewa katika fanali hizi za kombe la dunia.
.

No comments:

Post a Comment