Thursday, July 8, 2010

TUJIULIZE TUNAENDE WAPI?

Assalam aleykum

Tumetekwa na Ajenda za Siasa huku tukisahau wajibu wetu kuwatumikia Binadamu wenzetu khasa kuwapatia hifadhi Mayatima na Masikini.Nafasi ya kumtafuta nani awe mgombea imekuwa Muhimu zaidi ya kumtafuta nani wa kutunza Zakaah ili iwafikie Walengwa.

Pamoja na kuwa na UISLAAM zaidi ya Miaka elfu na ushee leo hii bado tunashindwa kuusimamisha kwa Vitendo Zanzibar. Wengine wakitafuta mbuzi wa kafara toka Dini zengine kuwasingizia Matatizo yetu ,wengine wakiwapachika mzigo huu wana Siasa wa Chama hichi au kile na kudhani kuna Chama fulani ndo jibu la Matatizo yetu.

Tukumbuke jibu la Umasikini wetu tunalo wenyewe,Jibu la kukosa Haki za Binadamu tunalo wenyewe na pia jibu la elimu Duni tunalo wenyewe. Tumekuwa Wateja wa itikadi za mivutano badala ya kuwa wenye Hisa kwenye Nchi yetu.

Tujiulize tunaenda wapi?

Zanzibar Zindabaad!

AMUR
.

No comments:

Post a Comment