
Akizungumza katika mahojiano na Shirika la habari la Marekani ,Associated Press mjini New York, waziri huyo alisema huenda serikali yake haiwapendezi baadhi ya watu , lakini haina upumbavu wa kufanya kitendo cha aina hiyo wakati mmoja.
Wakosoaji wanadai kwamba serikali ya Rwanda inawaandama na kuwakandamiza wapinzani kabla ya uchaguzi huo tarehe 9 mwezi ujao, wakitaja juu ya kuuwawa kwa mwandishi habari, Jean-Leonard Rugambage na kiongozi mmoja wa upinzani Andre Kagwa Rwisereka, na pia kupigwa risasi Jenerali wa zamani wa jeshi la nchi hiyo Kayumba Nyamwasa anayeishi uhamishoni Afrka kusini.
No comments:
Post a Comment