Tuesday, July 20, 2010

RWANDA YAKANUSHA INAWAANDAMA WAPINZANI

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Rwanda Louise Mushikiwabo,amekanusha kabisa kuhusika kwa serikali ya nchi yake katika mashambulio dhidi ya wapinzani watatu wa ngazi ya juu, akisema maafisa wa upelelezi na waandishi habari wanapaswa kuwasaka watu wanaojaribu kuzusha vurugu, kabla ya ya uchaguzi ujao wa rais.

Akizungumza katika mahojiano na Shirika la habari la Marekani ,Associated Press mjini New York, waziri huyo alisema huenda serikali yake haiwapendezi baadhi ya watu , lakini haina upumbavu wa kufanya kitendo cha aina hiyo wakati mmoja.

Wakosoaji wanadai kwamba serikali ya Rwanda inawaandama na kuwakandamiza wapinzani kabla ya uchaguzi huo tarehe 9 mwezi ujao, wakitaja juu ya kuuwawa kwa mwandishi habari, Jean-Leonard Rugambage na kiongozi mmoja wa upinzani Andre Kagwa Rwisereka, na pia kupigwa risasi Jenerali wa zamani wa jeshi la nchi hiyo Kayumba Nyamwasa anayeishi uhamishoni Afrka kusini.

No comments:

Post a Comment