Thursday, July 22, 2010

JINSI WENZETU WANAVYOJALI

Tukiangalia hii picha tutaona ni jinsi gani hawa wenzetu wazungu wanavyojali usalama wa mtu, hii sehemu tiles zake zilivunjika na wakazitoa lakini kwa kua bado hii sehemu hawajaitengeneza basi idara husika wameweka kizuizi ambacho kinamkinga mtu asije akakanyaga kwa bahati mbaya akaumia, lakini sisi nchini kwetu utakuta shimo kabisa liko kati kati ya barabara na hakuna ishara yoyote ambayo idara husika itaiweka kusudi iweze kumuonesha mtu kama pale pana jambo fulani la hatari, mpaka watu tu wenyewe wafanye kusaidiana kwa kuweka kitu kama majani ya mti, kwa kweli tuko mbali sana katika safari yetu.
Haya ndio mambo ya nyumbani wahusika hawana hata habari

No comments:

Post a Comment