Friday, June 11, 2010

ALIYEZIDIWA FURAHA NA KUMKUMBATIA KAKA

Nagery Ally Kondo (21) mwanafunzi katika shule ya Green Acres na mkazi wa Sekenke, Kinondoni jijini Dar Es Salaam, aliyeingia kiwanjani wakati mechi kati ya Tanzania na Brazili ikiendelea siku ya Jumatatu, Juni 7, 2010 ameachiwa huru na Jeshi la Polisi na kesi imeachwa mikononi mwa ofisi za shirikisho la soka Tanzania (TFF).

Kijana huyo alifika katika studio za redio Clouds FM na kuhojiwa katika kipindi cha Power Breakfast jana, Juni 10, 2010 na Dina Marios anaandika hivi katika blogu yake "...wakati wanaenda uwanja wa taifa yeye na wenzake walikata tiketi ya Tsh 30,000 lakini kutokana na kutokuwa na watu Maaskari waliwaruhusu kukaa jukwaa la Tsh 80,000....mpira ulipokolea Washikaji zake walimuona jamaa anavua mkanda, saa, viatu akawaomba wamshikie simu na kuwaambia mie naenda hivyo kumkumbatia Kaka.


Wenzie walijua utani mara jamaa akaanza kukimbia akielekea uanjani na kwenda kumkumbatia Kaka. Na anasema wakati anaenda alikuwa anajua lazima yatampata makubwa lakini alishaamua potelea mbali Mzuka wa soka ushampanda liwalo na liwe.

Anasema hakupanga chochote toka anatoka nyumbani mzuka ulimpanda wakati anangalia soka hapo uanjani na akajikuta anatamani kwenda kumkumbatia Kaka na ndicho alichofanya." - Dina Marios.

Watu kadhaa wametoa hisia mchanganyiko kuhusiana na tukio hili. Baadhi wamesema kuwa kwa kuwa alikuwa na nia njema na kwa kuwa kitendo kama hiki hutokea kwingineko duniani, basi adhabu yake isiwe ya kutisha. Wapo waliohoji umakini wa askari katiak kazi yao kuhusiana na hili.


Vile vile wapo waliasa kuwa endapo kijana huyu angekuwa ameficha silaha na kumdhuru yeyote kiwanjani, ingechafua kabisa nchi ya Tanzania na hili laweza kutokea kwani mtu anaweza kuficha silaha popote na kuitumia haraka.


No comments:

Post a Comment