Friday, June 11, 2010

MAHAKAMA NCHINI FINLAND YAMUHUKUMU KIFUNGO CHA MAISHA MCHUNGAJI WA RWANDA

Mahakama nchini Finnland imemhukumu kifungo cha maisha gerezani mchungaji Francois Bazaramba wa Rwanda.
Mahakama hiyo ya wilaya imemtia hatiani mchungaji Bazaramba kwa kushiriki katika mauaji ya kimbari yaliyotokea katika nchi yake aliyozaliwa mwaka 1994.

Katika hukumu yake, mahakama hiyo imesema hatua ya mchungaji huyo wa zamani inaonesha dhamira yake ya kuliteketeza kabila la Watutsi ama sehemu ya kabila hilo.

Televisheni za Finnland zimeripoti kwamba Bazaramba anapanga kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.

Polisi nchini Finnland walimkamata mchungaji huyo April mwaka 2007 kwa tuhuma za kushiriki katika mauaji hayo ambayo watu laki nane waliuawa.

No comments:

Post a Comment