Thursday, June 17, 2010

AGOMBEA URAIS ZANZIBAR SASA WAPIGWA MKWARA

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, kimesema marufuku kwa wanachama wake watakaojitokeza kuchukua fomu za kugombea nafasi ya urais kusindikizwa kwa mbwembwe za maandamano na wafuasi wao.

Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho, Saleh Ramadhan Ferouz, alipokuwa akizungumza na Nipashe kuhusu matayarisho ya zoezi la utowaji wa fomu linarotarajiwa kuanza wiki ijayo.

Alisema matayarisho yote yamekamilika na fomu zitaanza kutolewa Jumatatu ijayo kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa.

Aidha alisema wagombea wote watakao jitokeza watatakiwa kutoa taarifa siku moja kabla ya kuchukua fomu ili waweze kuingizwa katika ratiba badala ya kwenda ghafla.

“Wagombea wote watakao jitokeza kuwania urais wa Zanzibar hawaruhusiwi kusindikizwa kwa maandamano wakati wa kuchukua fomu na kurejesha” alieleza.

Alisema wagombea wote wanatakiwa kwenda kimya kimya wakati wa kuchukua fomu na kurejesha na wale watakaosindikizwa kwa mbwembwe za maandamano watakuwa wanakwenda kinyume na maadili ya chama kwa sababu wakati wa kampeni haujafika.

***Nipashe

No comments:

Post a Comment