Wednesday, February 24, 2010

U SHEIKH UKO WA AINA NYINGI

Ninavyojua mimi kuna vitu vitatu amavyo vinapelekea mtu kuitwa "Sheikh" na kama nitakua sijakosea, hii ndio kanuni haswa ya neno hili "Sheikh"

1. Mtu mzima aliyefikia makamo ya uzee.

2.Mtu mwenye fani (kazi) kama vile ufundi, udaktari, n.k.

3.Mtu mwenye elimu ya juu katika mambo ya dini ya Kiislamu.

Mambo hayo matatu mtu akiwa na moja kati ya hayo basi watu wanaweza kumpa au kumwita jina la "Sheikh", sasa hebu msikilize kwa makini huyu anaeitwa "Sheikh Yahya" ikisha utaniambia kaitwa

"Sheikh" kutokana na jambo lipi moja wapo?

2 comments:

  1. Huyu kaitwa Sheikh kutokana na hio fani yake ya ushirikina na wala si jengine

    ReplyDelete
  2. Neno sheikh ni neno la kiarabu,tafsiri yake ni kiongozi kwa kiswahili,kwa maana hiyo mtu yeyote alie kiongozi huitwa sheikh.kwa hiyo msifikirie sheikh ni mtu mcha mungu wa kiislam hapana. kwa hiyo huyo ni kiongozi wa USHIRIKINA na hivyo anavyo fanya uislam haukubaliani nae kwa mujibu wa ushahidi katika qur an;-BISMILLAH RAHMAN RAHIM. WAL MUSHIRIKINA FINNARI JAHHANNAM.TafsirI;-MSHIRIKINA(YOYOTE YULE)ATAINGIA MOTONI. Kwa hiyo huyo kiongozi yahya hussein akifa atakwenda MOTONI Labda atubu na aache kabisa ushirikina hapo anaweza kupata msamaha kwa MWENYEZI MUNGU. Mdau Leicester.

    ReplyDelete