Friday, February 26, 2010

TUDUMISHE MILA


Assalam aleykum

Enzi tulipokuwa wadogo, ilikuwa wali unapambiwa kwa mkungu, unafanya gamba (matandu) ya brown, mpunga mpya unanukia

Vile vile vijana walikuwa wanakung'utia maji ili yaonekane makaa yashamaliza kazi

Wapi, utamaduni umepotea! watu wote wanapiga rice cooker, wali si wali, bonndo si bondo, ni balaa tu.

Mchuzi pia ukipikwa kwa vyungu waweza ukajiramba, lakini wapi, watu wote tumejaa maluminium miili mwetu

Jee tunakwenda mbele au twarudi nyuma? Iko haja ya kudumisha mila.


***Mpitanjia

No comments:

Post a Comment