Monday, November 30, 2009

ZANZIBAR WACHEKA TANGANYIKA WALIA CHALLENGE

Mashindano ya Challenge yanaondelea kutimua vumbi huko Nairobi Kenya, Zanzibar wameanza vyema mashindano hayo kwa kuibugiza Burundi mabao 4-0 na kujiweka kwenye matumaini ya kuendelea na mshindano hayo huku Tanganyika ikianza vibaya mashindano hayo licha kuwa na wachezaji wao wanaochza soka ya kulipwa ulaya kwa kukamizwa mabao 2-0 na Uganda, nao Rwanda wakailaza Somalia kwa 1-0.
Kesho katika uwanja wa Mimius patakua hapatoshi wakati Zanzibar watakapokutana na Tanganyika huku Tanganyika wakitafuta matumaini ya kuweza kusonga mbele na Zanzibar wao pia wakitaka kujiongezea alama.

Leo hii kutakua na mechi kati ya Ethiopia wakiminyana na majirani zao Jibouti.

No comments:

Post a Comment