Saturday, November 28, 2009

WAINGIA IKULU BILA YA KUALIKWA

Wanandoa wawili Michele Salahi na mumewe Tareq walihudhuria chakula la jioni ndani ya Ikulu ya Marekani (White House) bila ya kualikwa, wanandoa hao walipata kupokelewa na rais Obama katika chumba cha mapokezi.Katika Ghafla hio ambayo ilihidhuriwa na wakuu mbali mbali akiwemo waziri mkuu wa india Manmohan Singh ambae alikua ndie mgeni rasmin katika ghafla hio

Bibi salahi alipata kupiga picha na wakuu mbali mbali waliohudhuria ghafla hio akiwemo makamo wa rais wa Marekani pamoja na kupenana mkono na Obama.

Wadadisi wa mambo wamesema kua kitendo cha wanandoa hao kutinga ndani ya White House kinyemela ni aibu sana kwa wanausalama wa ikulu hio, walinzi waliokua katika ghafla hio walikiri kufanya kosa kwa kuwaachia wanandoa hao kupita kiulaini.

Imesemwa kua hakukua na kitendo cha hatari ndani ya ikulu kufuatia kitendo hicho, uchunguzi zaidi unaendelea na bibi Salahi na mumewe Tariq wanaweza kushtakiwa ikiwa watabainika kutenda kosa

No comments:

Post a Comment