Thursday, November 26, 2009

48 WAFARIKI DUNIA KUTOKANA NA MVUA SAUDI ARABIA

Watu 48 wamefariki na wengine 900 wameokolewa baada ya mvua kubwa kunyesha huko SAudi Arabia. Msemaji katika wizara ya mambo ya ndani ya Saudi Arabia amesema hakuna katika majeruhi ambae ni miongoni mwa mahujaji waliohudhuria katika ibada ya hija.

Hija inajumuisha siiku nne ambayo ilianza siku ya jumatano na kuhudhuriwa na waumini milioni tatu kutoka kila sehemu duniani.

Mvua kwa sasa zimesimama lakini kuna matarajio ya mvua zaidi kunyesha,vyombo vya habari vimeripoti kua vifo vilitokea Jiddah, Rabigh na Makka.

Leo hii mahujaji wanafanya kitendo muhimu zaidi katika hija nacho ni kusimama katika mlima wa 'Arafa mpka jua kuzama.

Ibada ya hija mwaka huu inafanyika huku dunia ikiwa katika mgogoro mkubwa wa kiuchumi pamoja na mripuko wa homa ya mafua ya nguruwe (H1N1 virus)

No comments:

Post a Comment