Wednesday, November 11, 2009

ANUSURIKA KUFA BAADA YA KUANGUKA KWEYE NJIA YA TRENI

Mwanamke mmoja nchini marekani ambae alikua amelewa chakari alinusurika kufa baada ya kupepesuka na kuangukia katika njia ya treni, tukio hilo lilitokea katika kituo cha Nort Boston.

Mwanamke huyo alinusurika kufa baada ya watu waliokua wakisubiri treni kituoni hapo kusimamisha treni kwa kuipungia mikono baada ya kumuona mwanamke huyo ameanguka kwenye njia ya treni na kushindwa kuinuka kutokana na kuzidiwa na pombe kichwani, hata hivyo treni hio ilifanikiwa kusimama kabla ya kumponda mwanamke huyo.

No comments:

Post a Comment