Tuesday, June 15, 2010

Polisi yaahidi $6,250 kwa atakayetoa habari za mripuko, Kenya

Polisi nchini Kenya imeahidi kutoa zawadi kwa mtu atakayetoa habari kuhusu shambulio la grinedi katika mkutano wa hadhara wa kisiasa iliyowauwa watu 6.

Kamishna wa Polisi, Mathew Iteere, amesema kwamba anatarajia kwamba kima cha Dola 6, 250 kitaharakisha uchunguzi kuhusu shambulio la Jumapili katika mkutano wa kuipinga rasimu ya katiba.

Waliohudhuria mkutano huo wa hadhara wanaipinga rasimu hiyo ya katiba kwa sababu itahalalisha kutoa mimba katika hali hatari ya ujauzito na itatambua mahakama za Kadhi. Kura kuhusu rasimu hiyo itapigwa Agosti nne.

Bw. Iteere pia alisema polisi ilimkamata naibu waziri wa serikali pamoja na wabunge wawili kwa kutoa hotuba za uchochezi walipokuwa wanafanya kampeni dhidi ya rasimu hiyo ya katiba. Mashirika yasiyo ya kiserikali yanasema hotuba za uchochezi zilichangia ghasia za baada ya uchaguzi mwaka wa 2007 na 2008 ambapo kiasi ya watu 1000 waliuawa.
.

No comments:

Post a Comment