Wednesday, June 16, 2010

LAKERS WAIBUKA KIDEDEA "GAME 6" THE FINALS

Mechi ya 6 kati ya mechi 7 za fainali ya NBA kati ya Los Angeles Lakers na Boston Celtics imemalizika kwa Lekers kuibuka kidedea kwa kujipatia alama 89 dhidi ya 67 za Celtics.

Mechi ya leo ilikua ni vuta nikuvute kwenye robo ya kwanza lakini baada ya kuanza kwa robo ya pili timu ya Celtics walionekana kuzidiwa na kushindwa kufurukuta mbele ya wapinzani wao.

Ushindi wa leo kwa Lakers umewapa matumaini ya kuweza kuchukua ubingwa iwapo kama wataweza kushinda katika mechi ya saba ambayo pia wana matumaini nayo kwani mechi hio itachezwa katika uwanja wao wa nyumbani.

Kwa upande wake nyota wa timu ya lakers Kobe Bryant ikiwa kama watafanikiwa kunyakua taji hili la NBA basi itakua ni kwa mara ya tatu nje ya Shaquille O'neal na pia itakua ni kwa mara ya tano akiwa na timu hio ya LA Lakers.

Katika mechi ya leo Kobe Briant kama kawaida yake aliongoza kwa kupata alama nyingi kuliko mchezaji yoyote ambapo alipata alama 26 huku akifuatiwa na mchezaji wa Celtics Ray Allen ambae alipata alama 19.

Mechi sita za fainali za NBA "The Finals" hadi sasa zimekwisha chezwa ambapo matoke hadi sasa ni sare (3-3),na mechi ya saba na ya mwisho ya fainali hizi ambayo ndiyo itakayo amaua ni nani bingwa wa NBA 2010 inatarajiwa kuunguruma siku ya Alkhamis ya tarehe 17 mnamo saa 21:00 kwa Marekani ambapo itakua ni alfajiri ya kuamkia Ijumaa mnamo saa 03:00 (CET).
.

No comments:

Post a Comment