Monday, June 14, 2010

LA LAKERS WALALA TENA FAINALI NBA

Mchezo wa fainali ya kumtafuta bingwa wa mpira wa kikapu nchini Marekani kati ya Boston Celtics na LA Lakers umechezwa leo ambapo LA Lakers walishindwa kufurukuta dhidi ya Boston Celtics ambao waliutumia vyema uwanja wao wa nyumbani kwa kuwashinda Lakers kwa vikapu 92 kwa 86.

Mechi iliyochezwa leo ni ya tano kati ya mechi saba za fainali zitakazochezwa,ambapo mechi hio ilionekana ikiwa ni ya upande mmoja zaidi wakati Celtics walionekana kuudhibiti Mchezo na kuutawala katika vipindi vyote vinne.

Ushindi wa leo wa Celtics ni wa pili mfululizo huku ukiwa unafanya jumla ya ushindi wa mechi tatu za Celtics dhidi ya mbili kwa Lakers
Nyota wa kikapu wa timu ya Lakers Kobe Bryant aliweza kuipatia timu yake jumla ya alama 38, ambapo nyota wa upande wa Celtics Paul Pierce aliipatia timu yake jumla ya alama 27.
Alipohojiwa baada ya mechi hio Nyota Pul Pierce alisema " ilikua ni mechi yetu kubwa kwa mwaka huu, na kwa sasa tuko katika nafasi nzuri ambapo tuna michezo miwili huko Los Angeles na tunahitaji kushinda mmoja".
Celtics sasa inakua ni timu ya mwanzo kushinda mechi mbili mfululizo katika mechi zaba za fainali za NBA, na ikiwa kama Lakers hawataweza kushinda mechi mbili zilizobaki katika uwanja wao wa nyumbani basi Celtics watakua ni mabingwa.

Mechi ya sita ya fainali hio itachezwa siku ya Jumanne tarehe 15 mnamo majira ya saa 03:00 (CET) huko Los Angeles

.

No comments:

Post a Comment