Friday, June 4, 2010

JAJI NA KARANI WAKE WAPIGWA RISASI BRUSSELS

Mtu mmoja ambaye hakuweza kutambuliwa amempiga risasi jaji na karani wake katika chumba cha mahakama katikati ya mji wa Brussels nchini Ubelgiji jana.

Msemaji wa mwendesha mashtaka Jean-Marc Meilleur amesema mtu huyo mwenye silaha alikimbia na bado anatafutwa. Jean-Marc Meilleur anaamini kuwa mtu huyo bado ana silaha na hakuweza kuthibitisha iwapo amejeruhiwa.

Polisi wanaendelea na msako dhidi ya mtu huyo.

Haifahamiki kwa nini mshambuliaji huyo, ambaye amehudhuria kesi mahakamani hapo asubuhi ya jana pamoja na mawakili wawili, karani na jaji , aliwapiga wahanga hao wawili.

Waziri wa sheria Stefaan De Clerck amesema kuwa ni mara ya kwanza kwa jaji kuuwawa katika mahakama nchini Ubelgiji.
.

No comments:

Post a Comment