Friday, June 18, 2010

HATIMAE LAKERS WATETEA UBINGWA WAO "NBA"

Timu ya LA Lakers leo hii wamenyakua ubingwa wa NBA Basket ball baada ya kuwafunga Boston Celtics kwa jumla ya alama 83 kwa 79.


Mechi ya leo ilikua ni ya vuta nikuvute kwani tofauti na mechi sita zilizopita, hakukua na tofauti kubwa ya alama baina ya timu zote mbili.

Lakers leo hii wamejidhihirishia mbele ya Celtics kwamba wao ni mabingwa wa kikapu, kwani hadi robo ya tatu inamalizika Celtics walikua wanaongoza, lakini waliporudi uwanjani kumaliza robo ya nne hali ilianza kubadilika na hatimae kuibuka kidedea.

Ubingwa wa leo kwa Lakers utakua ni wa mara 16 nyuma ya Celtics ambao wamechukua kwa mara 17.

Mchezaji nyota wa NBA Kobe Bryant "The Black Mamba" kwa upande wake amefanikiwa kuchukua kombe hilo kwa mara ya 5 na hivyo kutangazwa kua MVP "most valuable player"

Katika mechi ya leo Kobe Bryant aliipatia timu yake ya Lakers jumla ya alama 23, ambapo wakati zilipokua zimebaki sekunde 90 mpira kumalizika Kobe aliiwezesha timu yake kuongoza kwenye kipindi cha pili kwa kuweza kupata alama kupitia "free throws".

LA Lakers watakua na furaha isio na kifani kwa kile kitendo cha kua nyuma kwa vipindi vya robo tatu kutokana na Celtics kua na Ulinzi wa hali ya juu lakini hatimae kuibuka kidedea katika robo ya mwisho.

Alipohojiwa baada ya mchezo Kobe alisema " tunapaswa kushinda na bahati sio inayonifanya mimi nifurahi, kinachonifanya mimi nifurahi ni Ushindi".
Kwa ushindi huu wa leo napenda kuwapa pole wapenzi wote wa Boston Celtics akiwemo Rafiki yangu Mwana a.k.a Chichi Heart akiwa maeneo ya Washington U.S.A.

No comments:

Post a Comment