Monday, June 14, 2010

CHAMA KINACHOTAKA KUJITENGA CHASHINDA UCHAGUZI BELGIUM

Chama kinachopigania kujitenga nchini Ubelgiji kimeshinda uchaguzi mkuu nchini humo.

Ushindi huo wa Chama hicho cha jamii ya waflemish cha N-VA katika uchaguzi uliofanyika mapema, kimeibua hofu kwamba huenda hali ya wasiwasi iliyotawala Ubelgiji, kwa miezi kadhaa itaendelea.

N-VA ambacho ni chama kinachopigania kujitenga kwa watu wanaozungumza lugha ya kiholanzi, kilipata ushindi mkubwa katika mkoa wa Kaskazini wa Flanders , ilhali chama cha Kisoshalisti kimepata ushindi katika mkoa wa Kusini wa Wallonia, eneo la wanaozungumza Kifaransa. Tofauti katika kugawana mamlaka baina ya mikoa hiyo miwili ndio ilikuwa sababu kuu ya kuanguka kwa serikali iliyopita ya mseto kabla ya muda wake kumalizika.

Vyama hivyo viwili vina misimamo tofauti ya kisera, lakini vinatarajiwa kuanza mazungumzo ya kuunda serikali ya muungano.
.

No comments:

Post a Comment