Wednesday, November 25, 2009

ZANZIBAR KWENDA KENYA KWA CHALLENGE

Wachezaji wa timu ya taifa ya Zanzibar wakiwa bandarini Dar-es-salaam leo asubuhi wakielekea nchini Kenya tayari kwa mashindano ya Challenge ambayo yatafanyika kwa muda wa wiki mbili.Safari hio imejumuisha watu 26 wakiwemo wachezaji 19 pamoja na viongozi 7.

Wachezaji ni pamoja na Abdi kassi,Mwadini Ali, Aggrey Morris, Suleiman Kassim, Abdallah Seif, Nassor Masoud, Sadik Habib, Ahmed Malik, Abdulhalim Humud, Abdulrahman Othman, Khamis Mcha, Haji Ramadhani, na Waziri Rajab.

Wengine ni Mohamed Salum, Rashid Faki, Nadir Haroub, Abdughany Gulam, na Mohamed Abdallah.


Viongozi ni pamoja na Hemed Suleiman Moroco (kocha msaidizi), Abdulfath Abbasi (kamati ya ufundi), Khamis Ali Mzee (mkuu wa msafara), Abdallah Saidi (daktari), and Haji Ameir (makamo wa rais ZFA).

Aidha jana ilianyika sherehe ya kuwaaga wachezaji hao ambapo katibu mkuu wizara ya habari utamaduni na michezo Omar Dadi Shajak aliwataka wachezaji hao ku jitahidi katika mashindano hayo ili kurudi na ushindi.


"Najua mtasafiri kutoka Dar-es-salaam hadi Nairobi kwa basi lakini hii isikuvunjeni moyo.


Ndugu Dadi alisema kua ni furaha kusafiri kwa basi kwani hata timu kubwa kama Manchester United pia wanatumia usafiri kama huo huko Ulaya,


"Serikali imetumia shilingi milioni kumi (10m.) kwa maandalizi ya timu, mnakwenda kuiwakilisha Zainzibar hivo ushindi wenu utatufanya sisi sote tujivunie"alisema katibu huyo kabla hajakabidhi bendera kwa nahodha wa timu hio.


Timu nyengine zitakazo shiriki mashindano hayo ni pamoja na Tanzania Mainland, hosts Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Ethiopia, Eritrea, Djibouti and Sudan.

No comments:

Post a Comment