Sunday, November 29, 2009

TIGER WOODS ATAFUTWA NA POLISI BAADA YA KUPATA AJALI

Bingwa namba moja wa golf duniani Tiger Woods anasakwa na Polisi wa mji wa Florida kwa ajili ya kufanya nae mahojiano kufuatia ajali ya gari aliopata siku ya ijumaa usiku Mnamo saa 2:25 am.Woods alipata ajali hio mara baada ya kushindwa kulimiliki gari lake alilokua akiendesha aina ya Cadillac 2009 na kwenda kugonga fire hydrant na baadae kugonga mti.

Katika ajali hio woods alipasuka mdomo na kutokwa na damu nyingi kitendo ambacho kilisababisha yeye kupoteza fahamu na kulazwa hospitali. lakini aliruhusiwa baada ya kupatiwa matibabu.
Mkuu wa polisi wa Windermere Chief Daniel Saylor,mke wa Woods bibi Elinaliiambia polisi kua alifika katika eneo la ajali na kumkuta mumewe amekwama ndani ya gari na hakuweza kumtoa kwa mlango wa mbele na ndipo alimtoa kwa kuvunja kioo cha nyuma ya gari kwa kutumia gongo la kuchezea golf.

Polisi walitarajia kuzungumza na Woods jana jumamosi lakini walimkosa walipofika nyumbani kwake, na katika mahojiano yaliofanywa na baba mkwe wa Woods ambae ni mtangazaji wa redio bwana Thomas Nordegren aliviambia vyombo vya habari kua hakua tayari kuzungumza kuhusu ajali

"sijazungumza nae ni siku sasa.....bwana thomas alisema kuhusu mwanawe Elin,kabla hajakata simu "sitaki kuzungumzia hili. Mama mkwe wa Woods pia alikataa kuzungumza kuhusu ajali hio.

Roger Federer ambae amekua rafiki mkubwa wa Woods katika miaka ya karibuni pia alisema kua hakuzungumza nae tangu alipotolewa nusu fainali ya ATP London " sijazungumza nae, lakini nasikia kama hayuko mahututi.

No comments:

Post a Comment