Monday, November 16, 2009

MASIKINI ZANZIBAR HAIKUA HIVI!!!


Picha hizi zinaonesha jinsi tamasha la muziki lijuilikanano kama Fiesta one love lililofanyika ngome kongwe Zanzibar na jinsi watu walivyovaa, kwa kweli nchi imefika pabaya sana.Sikusudii kusema kwamba Zanzibar kulikua hakuna miziki, nisieleweke vibaya. Zanzibar kuna miziki tangu mimi sijazaliwa lakini ilikua ni tofauti na hivi sasa.
Hapo zamani ilikua watu wakienda kwenye Taarab mziki ambao ndio unaopendwa sana Zanzibar, walikua wakivaa kwa heshima na hakukuwa na anaweza kuvaa nusu uchi,wala aneweza kukosa adabu, lakini picha hizi zinaonesha jinsi watu walivobadilika kiasi kikubwa katika mavazi, au hii ndio moja ya maendeleo?, kwa kweli inasikitisha sana kuona hali kama hii na mimi hua najiuliza bila kupata jibu kwamba je hawa watu ni wazanzibari au ni wageni wamekuja kwa sababu ya hilo tamasha? hapo silewi.
Kwa kweli jitihada inahitajika katika kurudisha hadhi na heshima ya Zanzibar, na ninaamini hakuna kinachoshindikana.

1 comment:

  1. Hawa wanaocheza miziki nusu uchi ni wabongo. Wanaletwa kusudi kuja kuharibu mila na silka za wazanzibari

    ReplyDelete