Monday, July 26, 2010

MOURINHO AMTAKA ASHLEY COLE

Kocha mpya wa timu ya Real Madrid Jose Mourinho ametangaza dau la Pound milioni 20 kwa mlinzi wa kushoto wa timu ya Chelsea Ashley Cole.

Mourinho alimshauri meneja wa Real Madrid Jorge Valdano huko Bernabeu kwamba wajaribu kutangaza dau hilo kwa timu ya Chelsea au kama itashindikana basi hata kwa kuingia mkataba wa kubadilishana na mchezaji ambapo Mourinho alimtaja kiungo mshambuliaji raia wa Uholanzi Rafael van der Vaartambae ndie atakae ingia katika mkataba wa kubadilishwa na Cole.

Vyanzo kutoka Real vimeeleza kwamba Mourinho anataka wachezaji ambao wana uzoefu kwa hivyo Ashley cole anafaa.
Kwa upande wake kocha wa timu ya Chelsea Carlo Ancelotti mpaka sasa ameonesha kutokubaliana na Mourinho kwa kumuuza Cole "kama mchezaji hajaridhika nitatumia njia ambayo itaweka mambo sawa lakini nafikiri Ashley atabaki kwa sababu hajawahi kusema kwamba hajaridhika" alisema Ancelotti.

No comments:

Post a Comment