Friday, June 25, 2010

WIMBI LA UKURASA MPYA ZANZIBAR

Assalam Aleykum!

Zanzibar inapita kipindi cha Wimbi la Political Stress ambayo hutokea kwa Nadra kwenye Historia.Zanzibar inakabiliwa na Mtihani Mgumu katika kuleta Mabadiliko ya Jamii yake.

Matokeo ya Kura za Maoni hapo 31.07.2010 ndio matokeo ya Rais Mtarajiwa ZNZ. Katika safu ya wale wa mwanzo yaani Maalim Seif , Balozi Karume na dr. Shein amejitokeza Bwa. Nahodha mwenye kuleta matumaini kwa kizazi kipya . Kati ya hao wote Bw. Nahodha ndie kijana waleo tukumbuke kuwa 2/3 ya Wapiga Kura ni kati ya miaka 18 na 45 ambao hawajayaona mapinduzi ya Jan 12 licha kuona Uhuru wa Dec.10. Mambo yanaweza kugeuka kuelekea kizazi kipya . Jee ndo tuseme YES WE CAN !! ipo ZNZ .

Jengine ni hili la Kura za Maoni

Tumebakiza wiki sita tu tufikie Kura za Maoni kuhusu Serikali ya Mseto kati ya Vyama vyenye Uwakilishi Barazani. Hii ni Neema kubwa kwani kumalizika kuundwa huko kwa Serikali ya namna hio kutafuata yale ambayo Wa-ZNZ tunayatarajia yaani Maendeleo na Amani Nchini mwetu. Tutaepukana na Sarakasi zisizoisha!! Inshallah . Ijapokuwa kula Mseto ni hiari sio lazima lakini tukae tukijuwa Mseto ni mtamu ukiwa ule tuliouzoea au ule wa Kande!
Call it what you will , the Rose smells sweet!!!

Wale ambao wanaosema Ndio tunawategemea kuwa Wingi Sana kuliko wanaosema Hapana kwani Wa-ZNz wanaitakia Umoja na Amaan Nchi mwao!!.

Zanzibar Zindabaad!!


***AMUR

No comments:

Post a Comment