Sunday, November 22, 2009

EMMA ANUSURIKA KWA MARA NYENGINE TENA BIG BROTHER

Mambo yamezidi kupamba moto ndani ya jumba la Big Brother, hivi sasa wamebaki washiriki 6 ndani ya jumba hilo baada ya mshiriki kutoka Nigeria Geraldine kufukuzwa kutoka kwenye jumba hilo kwa kupata kura chache huku Emma kunusurika kufukuzwa kwa mara nyengine tena baada ya kupata kura nyingi kumshinda Geraldine, kabla ya Geraldine kutolewa mjengoni IK alimtaka Itai kumtaja ni nani alie mnusuru na alimbadilisha na nani na ndipo aliposema kwamba amejinusuru yeye mwenyewe na amejibadilisha na Geraldine, na alipotakiwa kutoa sababu za kumuweka juu Geraldine alishindwa kufanya hivyo.

Kaa tayari kujua ni nani na nani atakua juu kwa kufukuzwa siku ya jumapili ijayo

No comments:

Post a Comment