
Timu ya Togo ilijiondoa katika mashindano ya Kombe la Afrika yaliyofanyika mapema mwaka huu nchini Angola, baada ya watu wawili wa ujumbe wao, pamoja na dereva wa basi lao kuuawa wakati timu hiyo iliposhambuliwa katika eneo la Cabinda.
Wakati ulimwengu mzima ulikuwa umeshtushwa na kusikitishwa na shambulio hilo, Togo ilipigwa marufuku kwa miaka minne, kwa sababu ya kujitoa katika mashindano bila ya kufuata taratibu.
.
No comments:
Post a Comment