
Waziri wa Fedha wa Uhispania, Elena Salgado amesema kiasi hicho kinaweza kuongezeka na kufikia Euro bilioni 720, pamoja na fedha za ziada kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF.
Fedha hizo zitatokana na Euro bilioni 440 zitakazotolewa na mataifa ya Umoja wa Ulaya yanayotumia sarafu ya Euro na mkopo mwingine wa Euro 60 utatolewa na Kamisheni ya Umoja wa Ulaya, huku Euro bilioni 220 zikitolewa na IMF.
Kamishna wa Umoja wa Ulaya anayehusika na masuala ya fedha na uchumi, Olli Rehn, amewaambia waandishi habari kuwa Umoja wa Ulaya utailinda na kuitetea sarafu ya Euro kwa namna yoyote ile.
Taarifa za mkopo huo wa fedha wa Umoja wa Ulaya umeisababisha Euro kuongezeka hadi dola 1.29 katika masoko ya fedha ya Asia hii leo.
.
No comments:
Post a Comment