Wednesday, September 30, 2009

MASHETANI WEKUNDU WACHARUKWA

Mashetani wekundu waendeleza rekodi ya kutofungwa nyumbani kwa mechi za Champions League tangu 2005 kwa kuikandamiza Wolfsburg 2-1, mabao ya mashetani wekundu yamewekwa nyavuni na Gigs huku bao la pili likapachikwa na Carrick.
Matokeo mengine ni kama ifuatavyo

Milan 0-1 Zurich
Bayern 0 - 0 Juventus
Bordeaux 1 - 0 Maccabi Haifa
Real Madrid 3 - 0 Marseille
Porto 2 - 0 Atletico Madrid
APOEL Nicosia 0 - 1 Chelsea
CSKA Moscow 2 - 1 Besiktas Soma Zaidi ...

MAANDAMANO YA CUF YATIKISHA JIJI LA DAR

Fanya Fujo Uone wakihakikisha usalama unapatikana katika maandamano hayo
Wananchi wakisikiliza kwa makini hotuba baada ya maandamano
Wananchi wakikatisha katika mtaa wa Msimbazi Kariakoo
Chama cha wananchi CUF leo wamelitikisha jiji la Dar kwa kufanya maandamano ya aina yake, maandamano hayo yalikua na lengo la kudai tume huru na ya haki katika uchaguzi mkuu nchini,maandamano hayo yalianzia Buguruni na kumalikia katika viwanja vya kidongo chekundu
Soma Zaidi ...

CHAMPIONS LEAGUE LEO HII

17:30CSKA Moscow vs Besiktas
19:45Bayern vs Juventus
19:45Bordeaux vs Maccabi Haifa
19:45Manchester United vs Wolfsburg
19:45Real Madrid vs Marseille
19:45Milan vs Zürich
19:45Porto vs Atletico Madrid
19:45APOEL Nicosia vs Chelsea

Note: GMT+(01:00)
Line up ya Mashetani wekundu inatarajiwa kama ifuatavyo:-
1.Foster
2.O'shea
3.Evra
4.Evans
5.Vidic
6.Anderson
7.Valencia
8.Fletcher
9.Owen
10.Barbatov
11.Prk
MANU leo watacheza kwa Formula ya 4-4-2 wakati Wolfsburg watachekwa kwa 5-3-2

MANU hawajapoteza mchezo wowote wa nyumbani kwa mechi za Champions League tangu walipofungwa na AC Milan 1-0 2005,lakini wakati huo huo Wolfsburg wamepoteza mechi moja tu kati ya mechi nne za nje walipocheza UEFA Cup 2008/09.
Soma Zaidi ...

JK ATEMBELEA OFISI ZA BUNGE US


JK alipokutana na Spika wa bunge la marekani bibi Nancy Pelosi afisini kwake Washington DC.
Soma Zaidi ...

Soma Zaidi ...

KUMBE KILA KITU KINAWEZEKANA

Hatimae kilio cha wanafunzi wa skuli ya kibasila kupitia maandamano waliyoyafanya chasikilizwa. serikali imekubali kukaa chini na kuzungumza na wanafunzi hao na kukubaliana kuweka matuta eneo la skuli hio kwa kupunguza ajali za mara kwa mara zinazotokea skulini hapo. sasa mimi hapa ndio hujiuliza, kumbe kama kusingekua na maandamano wanafunzi hao wangeendelea kuuwawa kwa ajali kila siku,

mhhh nakosa jibu

Soma Zaidi ...

Tuesday, September 29, 2009

HAHAHAAAAAAAAAA!!!!! LIVERPOOL TAABANI KWA FIORENTINA


Timu ya liverpool leo imejikuta si lolote si chochote dhidi ya fiorentina baada ya kukandamizwa bila ya huruma mabao 2-0 kwa kweli liverpool wanahitaji mazoezi ya ziada ili kujiandaa na Chelsea jumapili ijayo Soma Zaidi ...

TAIFA QUEENS WATOKA SARE NA AFRIKA KUSINI


Mchezaji wa Afrika kusini Mampho Tsotetsi akiangalia ni nani wa kumpasia mpira huku mchezaji wa Taifa Queens Jackline Sakozi akimkaba kwa makini ili asije akaleta madhara. mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya 31-31.
Soma Zaidi ...

CHAMPIONS LEAGUE INAENDELEA USIKU WA LEO

 17:30 Rubin v Internazionale Central, Kazan
 19:45 Fiorentina v Liverpool Stadio Artemio Franchi, Florence
 19:45 Debrecen v Lyon Ferenc Puskás-Stadion, Budapest
 19:45 Barcelona v Dynamo Kiev Camp Nou, Barcelona
 19:45 Rangers v Sevilla Ibrox Stadium, Glasgow
 19:45 AFC Unirea Valahorum Urziceni v Stuttgart Stadionul Ghencea, Bucharest
 19:45 Arsenal v Olympiacos CFP Emirates Stadium, London
 19:45 AZ v Standard Liège DSB Stadion, Alkmaar

  Note: kwa saa za bara ulaya
Line up ya Liverpool leo hii itakua ni
1)Reina
2)Johnson
3)Insua
4)Skrtel
5)Carragher
6)Lucas
7)Kuyt
8)gerrard
9)Torres
10)Babel
11)Riera
Liverpool wanatarajiwa kucheza kwa formula ya 4-5-1 wakati Fiorentina watacheza kwa 4-4-2

                                                                                                                        
Soma Zaidi ...

JINSI KI INGLISH KISIVO NA THAMANI ULAYA NJE YA UK

Guido Westerwelle, ambae inatarajiwa sana kuwa ndie atakaekua waziri wa mambo ya nchi za nje wa kijerumani katika serikali ijayo,alikataa kuulizwa swali kwa kiengereza baada kwa kumkumbusha  mwandishi wa habari ambae alimuuliza swali kwa lugha ya kiengereza, alisema "tupo Ujerumani hapa"jibu hilo lilikuja baada ya mwandishi mmoja wa BBC kumuuliza kama je angeweza kujibu swali la kiengereza?, lakini bwana Westrewelle alijibu sali hilo kwa lugha ya kijerumani. Mwandi huyo wa BBC aliuliza tena swali kama je anaweza kuuliza swali kwa kiengereza na yeye akajibu kwa kijerumani?ndipo Bwa Westernwelle alipomwambia kama "England watu wanazungumza kiengereza, kwa hio ni sawa na hapa watu wanazungumza kijerumani" alisema kwa lugha ya kijerumani. Soma Zaidi ...

MWAKILISHI WA CUF APANDISHWA KIZIMBANI

Mwakilishi wa chama cha wananchi ( CUF ) jimbo la chonga kisiwani pemba Mh Abdallah Juma Abdallah jana amepandishwa mahakamani katia mahakama ya mwanzo Wilaya ya Chake Chake kwa kosa la kumtolea maneno ya kashfa na matusi sheha wa shehia ya Pujini Bwana Khamis uledi kombo, katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Chake Chake kufuatia utoaji wa vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi (Zan IDs). Mwendesha mashtaka Bwana Juma Habib aliiambia mahakama hio kwamba mwakilishi huyo alitenda kosa hilo siku ya tarehe 19 aug, mwaka huu na kutiwa hatiani kwa kifungu cha sheria  ya Zanzibar 74(1) (b) ya mwaka 2004 Hata hivyo mwakilishi huyo alikanusha kosa hilo na hakimu wa mahakama hio Ali Abdurrahman Ali alimwachia kwa dhamana ya sh,150,000 na kesi kuhairishwa hadi tarehe 15 oct 2009 itakaposikilizwa tena.
Soma Zaidi ...

Mjane Maria Nyerere akiwaonesha waandishi wa habari cheti pamoja na medali alizotunukiwa na Rais wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa ( UNSC ) father Miguel D'Escoto Brokmann New York hivi karibuni.Tunzo hizo zilitolewa kwa kutambua mchango wa Mwalim Nyerere katika harakati za kupigania uhuru wa bara la Afrika. Kushoto ni mwanawe Makongoro Nyerere
Soma Zaidi ...

WIKI YA USLAMA BARABARANI YAANZA


Asakari wa usalama barabarani akiongoza magari katika barabara ya kinondoni makutano ya Ali Hassan Mwinyi Road kufuatia wiki ya usalama barabarani. Wiki ya usalama barabarani ilianza rasmin jana nchi nzima
Soma Zaidi ...

JK AFUNGUA RASMIN JENGO LA UBALOZI WASHINGTON DC




Rais kikwete amefungua rasmin jengo la ubalozi wa tanzania nchini Marekani ambalo lipo katika jiji la Washington DC. Jengo hilo ambalo serikali imelinunua limegharimu kiasi cha dola za kimarekani $ 10,415,000.
Soma Zaidi ...

JEE HAWA WANAE ANGALAU MBUNGE WA KUWAANGALIA?


Soma Zaidi ...

Monday, September 28, 2009

MANCHESTER CITY WAIKANDAMIZA WEST HAM 3 - 1

      

Timu ya manchenster City leo imeikandamiza mabao 3 - 1 timu ya West Ham, bao la kwanza la City lilifungwa na Carlos Teves, la pili likafungwa na Martin Petrov kwa njia ya free kick na baadae Carlos teves tena kwa kumalizia bao la tatu, na bao la kufutia machozi la West Ham lilifungwa na Carton Cole Soma Zaidi ...

WANAFUNZI SKULI YA KIBASILA WAANDAMANA NA KUFUNGA NJIA YA CHANG'OMBE NA MANDELA ROAD

Wahusika katika jeshi la polisi walifika eneo la tukio na kujadiliana juu ya nini cha kufanya


Jinsi walivokua wamekaa barabarani hapo kama vile hakuna jambo lolote linaloendelea


waliamua kuimba na kucheza barabarani hapo



Wanafunzi katika shule ya kibasila mijini Dar-es-salaam waliandamana leo mchana na kufunga barabara ya chang'ombe na Mandela road kufuatia ajali za mara kwa mara kwa wanafunzi katika eneo hilo.
Wanafunzi hao wamenzisha maandamo hayo ambayo hayakua na kibali kutoka kwa wakuu wa skuli, jeshi la polisi wala kutoka kwa mkuu wa wilaya.
Wanafunzi hao walidai kwamba hawataondoka sehemu hio hadi pale wahusika wakuu watakapo kuja na kuzungumza nao ili kutoa tamko rasmi la kuwekewa alama za barabarani katika eneo hilo, barabara hio haina alama yeyote ya na hivo kusababisha vifo vya kila siku kwa wanafunzi wa skuli hio.





Soma Zaidi ...

JAMAA AOWA WAKE WANNE KWA WAKATI MMOJA SOUTH AFRICA


Mhhhh! ni mambo ya economy crisis Soma Zaidi ...

MWANAMKE WA KIZANZIBARI KATIKA VAZI LA KANGA

Hivi ndivo anavoonekana mwanamke wa kizanzibari akiwa amevalia vazi maarufu la kanga visiwani humo na kanga hizi zinajuilikana kwa jina la (mapembea) Soma Zaidi ...

Kipindu pindu chauwa Zanzibar

Watu watatu wanasadikiwa kufariki dunia na wengine wapatao 20 kulazwa katika kambi maalum zilizopo mtopepo kutokana na maradhi ya kipindu pindu. Soma Zaidi ...